Kaunti ya Kirinyaga inaongeza juhudi za kuwawezesha vijana kwa ujuzi wa kidijitali, huku vijana sitini wakihitimu kutoka Chuo cha Ufundi cha Kilimo cha Kaunti katika masomo ya Kompyuta.
Mhafali hao, waliotoka Wadi ya Karumandi, ni kundi la kwanza chini ya programu iliyoidhinishwa na TVETA inayounganisha ujuzi wa kidijitali na kilimo pamoja na sekta nyingine zinazoibuka. Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyofanyika Kamweti, waziri wa kilimo w kaunti hiyo John Gachara alisema kuwa teknolojia sasa ni kiini cha kilimo cha kisasa.