Wanamibia wafurahia kuchaguliwa rais wa kwanza mwanamke
Netumbo Nandi-Ndaitwah amekuwa mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kuwa rais nchini Namibia.
Nandi-Ndaitwah, mwenye umri wa miaka 72, aligombea urais kwa chama kinachotawala cha SWAPO.
Ushindi wake utaendeleza uitawala wa miaka 34 wa SWAPO madarakani, tangu Namibia ilipopata uhuru kutoka kwa Afrika kusini mwaka 1990.
Tume ya uchaguzi ya Namibia imetangaza matokeo rasmi yanayoonyesha kwamba amepata asilmia 57 ya kura.
Kulingana na katiba ya Namibia, mshindi wa kura za urais anahitajika kupata asilimia 50 ya kura.
Baada ya kutangazwa mshindi, Nandi – Ndaitwah amesema kwamba wapiga kura wa Namibia wamechagua amani na utulivu.
Amekuwa mwanachama wa SWAPO tangu miaka ya 1960 wakati chama hicho kilikuwa kinapigania uhuru na amehudumu katika nafasi mbalimbali za ngazi ya juu serikalini ikiwemo waiziri wa mambo ya nje.
Mshindani wake mkuu Panduleni Itula, wa chama cha Independent Patriots for Change (IPC), amemaliza katika nafasi ya pili kwa akiwa na asilimia 29 ya kura.
Chama cha IPC kimedai udanganyifu katika uchaguzi huo na kimesema kitapinga matokeo mahakamani.
Uchaguzi wa Nove 27 ulikumbwa na matatizo ya kiufundi na uhaba wa karatasi za kupigia kura na kupelekea matokeo kuchelewa kutangazwa.
- Vyanzo mbalimbali
#NetumboNandiNdaitwah #namibia #SWAPO #rais #uchaguzi #voa #voaswahili
17 Jun 2025
- Gachagua has torn into President Ruto for what he terms as a disregard for human life.
17 Jun 2025
- The mask vendor was unarmed and shot in full glare of the public.
17 Jun 2025
- One person was shot by police at point-blank range, amid allegations police turned a blind eye to armed goons who attacked protesters.
18 Jun 2025
- KNCHR has recorded 22 casualties during the Tuesday demonstrations calling for the resignation of Deputy Police Inspector General Eliud Lagat over his alleged involvement in teacher Albert Ojwang's murder.
18 Jun 2025
- Today’s protests took a sinister turn as police officers and hired thugs joined forces in plain sight. In a scene both brazen and unsettling, hired goons arrived on motorbikes, others armed with clubs and whips terrorizing innocent passers-by all under…
17 Jun 2025
- What had been intended as protests to demand accountability over the murder of teacher Albert Ojwang in police custody last week turned into an all-out clash pitting three groups: the police, protesters and hired goons.
17 Jun 2025
- The police officer who shot an unarmed mask vendor during the demonstrations held in Nairobi on June 17, 2025, has been arrested.
17 Jun 2025
- At around 10 p.m. on a cold night, a sudden sharp pain on the right side of her stomach sent 22-year-old Vestina Samson to the ground. Writhing in pain, Vestina’s family was unsure how to help her.
17 Jun 2025
- Three officers, among them the Officer Commanding Station at Mawego Police Station, where the late Albert Ojwang’ was briefly held before his controversial transfer to Nairobi, have now recorded statements as investigations gather pace.
17 Jun 2025
- The streets of Nairobi on Tuesday were nothing short of lawless as police officers worked with goons to fight off protesters.
17 Jun 2025
- “The nation is reeling from the deeply troubling shooting of an unarmed civilian.”
17 Jun 2025
- The tragic road accident along the Bondo-Kisian road also left 30 others injured
17 Jun 2025
- Injuries range from gunshot wounds, head cuts, whip lashes and blunt trauma