- 542 viewsDuration: 2:27Waziri wa kawi na petroli Opiyo Wandayi ameagizwa kufika mbele ya kamati ya kawi katika bunge la kitaifa kuhusiana na sakata ya mafuta inayoendelea. Wandayi akiagizwa kufika kufafanua yale anayoyajua kuhusiana na sakata hii iliyosababishwa kujiuzulu kwa maafisa kadhaa wakuu kwenye wizara hiyo. Haya yanajiri huku halmashauri ya kuthibiti bei ya mafuta nchini EPRA ikitishia kubatilisha leseni za kampuni zinazoficha mafuta na kuhakikisha kuwa Kenya bado ina mafuta ya kutosha