- 229 viewsWatu kadhaa wamekamatwa na kuzuiliwa kufuatia vurugu zilizozuka huko busia. Maandamano yalizuka mjini kufuatia kutoweka kwa mfanyibiashara,Ibrahim Mohammed, kwa wiki mbili sasa . Wakazi na familia ya mfanyibiashara wanataka polisi kutoa taarifa kuhusu aliko, wakidai kuwa alitoweka muda mfupi baada ya kushushwa kwenye basi katika kizuizi cha polisi.