Ajali za barabarani zimeendelea kusababisha vifo vya watu karibu kila siku katika msimu huu wa sikukuu, licha ya wito kwa madereva kuwa waangalifu zaidi. Katika tukio la hivi punde lililoripotiwa, watu watatu walifariki papo hapo baada ya gari aina ya Toyota Probox walilokuwa wakisafiria kugongana ana kwa ana na trela katika eneo la Kedowa kando ya barabara kuu ya Kericho–Nakuru, alfajiri ya siku ya Krismasi. Polisi wanadai kuwa dereva wa gari hilo alikuwa akiendesha gari akiwa mlevi.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive