- 426 viewsDuration: 3:18Shule zaidi ya kumi zimesalia mahame miaka mitatu baada ya mashambulizi katika maeneo bunge ya Turkana mashariki na kusini. Madarasa yameachiwa vichuguu, viwanja vya shule vikageuka vichaka vya wanyama na Kumbi kusalia na kimya cha makaburini. Hii ni licha ya serikali kuu kuahidi kuwatuma wanajeshi kukarabati shule zilizovamiwa na kuteketezwa na wahalifu.