- 12,283 viewsDuration: 3:51Kesi ya uhaini inayomkabili mwenyekiti wa chama cha demokrasi na maendeleo CHADEMA Tundu Lissu imeahirishwa hadi siku ya jumatano tarehe 11 ya mwezi huu wa Februari ambapo itatajwa tena, huku mahakama hiyo ikitarajiwa kutoa uamuzi kuhusu pingamizi la Lissu la kuwaficha mashahidi wa siri. Lissu aliiambia mahakama mwaka jana kuwa kuwaficha mashahidi hao kunawanyima hata majaji nafasi ya kuwaona jambo ambalo ni kinyume cha sheria, na kusisitiza kuwa yote hayo ni kwasababu kesi inayomkabili hukumu yake ni kunyongwa hadi kufa. #tundulissu #bbcswahili #tanzania #bbcswahilileo Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw