- 964 viewsDuration: 1:36Viongozi wa jamii za Ameru na Somali wanaoishi katika kaunti ya Garissa wameahidi kuishi kwa amani na kumaliza uhasama wao kwa kutangamana na kufanya biashara pamoja. Wakizungumza wakati wa kutawazwa kwa viongozi wa jamii ya Ameru mjini Garissa, viongozi hao walisifia historia ndefu ya jamii hizo na kuwasihi viongozi wapya kutatua mizozo ndogo ndogo miongoni mwa jamii hizo bila kuleta chuki kati yao. Viongozi wa Ameru walihimiza kuimarishwa kwa biashara ya miraa bila kutozwa ada za kiholela na serikali za kaunti kwenye vizuizi zinazowekwa barabarani.