- 622 viewsDuration: 1:38Baadhi ya viongozi wa eneo la Ukambani wanaogemea upande wa serikali wamemtetea waziri wa afya Aden Duale kutokana na shinikizo za wenzao wanaosema wanapanga kumbandua mamlakani kwa sakata ya bima ya SHA. Wanasiasa hawa wakijumuisha Vincent Musyoka wa Mwala na seneta mteule Tabitha Mutinda wanasema wanaomtaka Duale kuondoka ni wanafiki wakitetea hatua za Duale kulainisha bima hiyo. Walikuwa wakizungumza wakati wa hafla ya kuchangisha pesa kwa sekta ya bodaboda eneo la Kitui Mashariki