- 798 viewsDuration: 2:11Familia za waathiriwa wa maandamano ya Gen Z waliotoweka wameendelea kuitaka serikali kuwajibikia swala hili na kutoa taarifa za waliko jamaa zao. Ingawa imekuwa miaka miwili tangu kutoweka kwa baadhi yao, familia hizi zinasema zina matumaini kuwa jamaa zao watarudi siku moja. Na kama Brenda Wanga anavyoarifu, mashirika ya haki sasa yanataka bunge kupitisha kwa haraka sheria kuhusu watu wanaopotezwa kiholela.