- 361 viewsDuration: 1:48Magavana Simon Kachapin wa West Pokot na Ken Lusaka wa Bungoma wamewahimiza wawekezaji kuongeza uwekezaji katika sekta ya hoteli na utalii, wakisema inachangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa uchumi kupitia serikali za ugatuzi. Wakizungumza mjini Kitale baada ya kuzindua rasmi hoteli ya Saiwa Safari, viongozi hao walisema sekta hiyo huchangia mamilioni ya pesa katika mapato ya kaunti, kubuni nafasi za ajira kwa vijana na husaidia kutangaza vivutio vya utalii.