- 3,829 viewsDuration: 3:13Idara ya polisi inaendelea na uchunguzi wa vurugu zilizoshuhudiwa katika mkutano wa kisiasa ulioongozwa na Naibu Rais Kithure Kindiki huko Embu siku ya Jumamosi. Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Gilbert Masengeli amelaani kuenea kwa visa vya uhuni, akisema polisi watakabiliana na wahuni wanaovuruga mikutano ya kisiasa. Haya yanajiri huku familia ya Mike Lewis Macharia, anayedaiwa kupigwa risasi wakati wa ghasia hizo, ikiendelea kutafuta haki.