- 1,717 viewsDuration: 1:18Waziri wa Utumishi wa Umma Geoffrey Ruku leo amefika mbele ya Tume ya Kitaifa ya Uwiano na Utangamano (NCIC) kujibu maswali kuhusu madai ya kueneza chuki kupitia matamshi yake katika eneo la Mlima Kenya. Ruku alihojiwa na NCIC huku akisisitiza kuwa viongozi wote walioitwa na tume hiyo wanapaswa kufika na kujibu maswali. NCIC inatarajiwa kutoa mwelekeo wake kuhusu suala hilo baada ya wiki moja. Gavana wa Busia Paul Otuoma na Mbunge wa Homa Bay Peter Kaluma pia walihojiwa na tume hiyo Jumatatu.