- 12,604 viewsDuration: 1:10Wanasiasa wa Linda Mwananchi walilazimika kukatiza mkutano wao kwa muda katika Kaunti ya Meru, baada ya vitoa machozi kurushwa kuwatawanya wafuasi na viongozi hao. Haya yakijiri huku mgawanyiko ukijitokeza kwenye mrengo huu kuhusu ni nani anayepaswa kubeba bendera ya kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu ujao. Viongozi waliofanya kampeni maeneo ya Meru wakitangaza kumuunga mkono Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, wakipuuza tangazo la Gavana wa Siaya James Orengo kuwa atawania urais. Seth Olale anaarifu.