- 1,293 viewsDuration: 2:53Washukiwa watatu wanaotuhumiwa kuhusika na mauaji ya Daktari Victoria Mutiso watazuiliwa kwa siku thelathini zaidi kuruhusu upande wa mashtaka kukamilisha uchunguzi. Katika uamuzi wake, hakimu mkuu mwandamizi wa mahakama ya Milimani Teresia Nyagena ameagiza watatu hao wazuiliwe katika vituo vitatu tofauti katika muda huo. Afisa wa polisi Collins Bett na Pius Muiru walikamatwa nchini Uganda wiki iliyopita huku mshukiwa wa tatu aliyetambuliwa kama Samuel Karanja akikamatwa jijini Nairobi.