Wachimba migodi haramu wafariki katika machimbo ya madini
Watu 100 ambao walikuwa wakichimba madini kinyume cha sheria katika mgodi wa dhahabu usiofanya kazi nchini Afrika Kusini walifariki baada ya kunaswa chini ya mgodi huo kwa miezi kadhaa, huku polisi wakijaribu kuwaondoa huko, kundi linalowakilisha wachimba migodi hao lilisema Jumatatu.
Sabelo Mnguni, msemaji wa jamii zilizoathiriwa na uchimbaji madini aliliambia shirika la habari la Associated Press kwamba simu ya mkononi iliyotumwa juu ya mgodi huo na baadhi ya wachimba migodi waliookolewa siku ya Ijumaa, ilikuwa na video mbili zikionyesha miili kadhaa iliyofunikwa kwa plastiki chini ya ardhi.
Mnguni alisema “takriban watu 100 walifariki katika mgodi katika mkoa wa kaskazini magharibi ambako polisi walianzisha operesheni mwezi Novemba kuwalazimisha wachimba migodi kuondoka.
Wanashuku watu hao walikufa kwa njaa au kwa sababu ya kukosa maji mwilini, Mnguni alisema.
Alisema miili 18 iliondolewa ndani ya mgodi huo tangu Ijumaa.
Msemaji wa polisi Brigedia Sebata Mokgwabone alisema bado wanachunguza taarifa kujua ni miili mingapi iliyopatikana na ni manusura wa ngapi waliookolewa baada ya operesheni ya uokoaji kuanzishwa Jumatatu.
-AP
#Stilfontein #madini #mgodi #dhahabu #wachimbaji #afrikakusini #wachimbajiharamu #voa #voaswahili
17 Jun 2025
- The agency also issued prospective applicants of the way forward.
17 Jun 2025
- Only 2 nations beat Kenya, according to a new study.
17 Jun 2025
- Kioni's response comes days after Moses Kuria expressed interest in the Jubilee Secretary General position ahead of 2027.
17 Jun 2025
- The victim, identified by locals as Moureen, was found lying in a pool of blood with her throat slit, prompting widespread shock and outrage in the quiet village.
17 Jun 2025
- Suba North Member of Parliament (MP) Millie Odhiambo has called for thorough investigations into the alleged suicide incident of arrested fisherman at Kipasi police post in Suba North constituency on Sunday.
17 Jun 2025
- The national government has launched a Ksh.60 million relief programme for Tana River residents affected by perennial flooding.
17 Jun 2025
- Ugandan President Yoweri Museveni has signed legislation that allows military tribunals to try civilians, parliament said on Monday, a move opposition leaders said violates a Supreme Court ruling.
17 Jun 2025
- Ugandan President Yoweri Museveni has signed legislation that allows military tribunals to try civilians, parliament said on Monday, a move opposition leaders said violates a Supreme Court ruling.
17 Jun 2025
- The agency also issued prospective applicants of the way forward.
17 Jun 2025
- Only 2 nations beat Kenya, according to a new study.
17 Jun 2025
- DCI officer says Albert Ojwang's arrest was carried out on the orders of Mr Amin Mohammed.
17 Jun 2025
- The Pharmacy and Poisons Board (PPB), in collaboration with the Global Health Protection Programme (GHPP)–PharmTrain2 initiative, has kicked off a five-day regional workshop aimed at strengthening regulatory capacity in the assessment of bioequivalence…
17 Jun 2025
- For the longest time, there have been intensified calls for human rights. Rights for the girl-child, the youth, gender inequality, climate change, and all that. These calls have been intensified as individuals, organisations, and civic groups keep…