- 1,190 viewsDuration: 2:58Wakazi na viongozi wa eneo la magharibi, hususan kutoka kaunti za vihiga na trans nzoia, wameomboleza kifo cha mwanasiasa cyrus jirongo, wakimtaja kama mtu aliyetoa mchango mkubwa katika maendeleo ya eneo hilo na aliyekuwa mkarimu kwa watu wote. Nyumbani kwao katika kaunti ya vihiga, waliotangamana naye wamemtaja kama kiongozi ambaye hatakuwa rahisi kurithiwa, kutokana na kujitolea kwake kwa maendeleo ya ukanda wa magharibi.