- 2,410 viewsDuration: 2:48Mwanamume mmoja katika eneo la Freer Town Kaunti ya Mombasa analilia haki baada ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi miezi miwili iliyopita. Omar Ali anadai kuwa masaibu yake yalianza alipolazimishwa kutia saini stakabadhi kuonyesha kuwa alikuwa amekubali kuondoa kesi na maafisa hao waliompiga risasi walipokuwa wakishika doria eneo hilo mwezi Oktoba. Omar anasema juhudi zake za kutafuta haki na kuripoti polisi pia zimegonga mwamba.