- 6,312 viewsDuration: 2:01Mtu mmoja amefariki katika mkasa wa moto ulioteketeza nyumba sita katika eno la Millenium mjini Diani kaunti ya Kwale. Inasemekana mwanamke huyo wa miaka arobaini alipiga kamsa majira ya saa tisa alfajiri ya leo baada ya nyumba yake kushika moto kabla ya keuenea hadi nyumba zingine. Wakaazi hawakufaulu kumuokoa kutokana na makali ya moto huo ulioteketeza mali yote katika nyumba hizo. Bado chanzo cha moto hakijabainika wenyeji wakitaka serikali kuwasaidia walioathirika.