- 429 viewsDuration: 1:40Ujenzi wa kituo cha kuhifadhi gesi ya bei nafuu ya Taifa Gas katika eneo la kibiashara la Dongo Kundu umefikia asilimia 80. Katibu katika idara ya uwekezaji Abubakar Hassan Abubakar amesema kituo hicho kitazinduliwa mwezi Machi mwaka huu ili kuanza kusambazia wananchi gesi hiyo. Kituo hicho kinachogaharimu takriban shillingi billioni 16 kitakua na uwezo wa kuhifadhi tani 30,000 hadi 45,000 za gesi na kubuni nafasi zaidi za ajira.