Katibu katika wizara ya usalama wa taifa Dkt. Raymond Omollo, amesema serikali itaendelea kutekeleza mpango wa ajenda kumi ulioafikiwa na kamati ya mazungumzo ya kitaifa (NADCO) pindi tu kesi zilizo mahakamani zitakapokamilika. Alisema serikali inataangazia kuwafidia waathiriwa wa ukiukwaji wa haki za binadamu wa zamani. Omollo alisisitiza kuwa serikali ya Kenya Kwanza chini ya Rais Ruto haitatelekeza ripoti ya NADCO licha ya changamoto za kisheria, na kwamba haki kwa waathiriwa na familia zao bado ni jambo la muhimu sana. Wycliffe Oketch na taarifa kamili.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive