- 267 viewsDuration: 3:19Wafanyabiashara katika Soko la Kiminini, Kaunti ya Trans Nzoia, wamesifia hatua ya kupandishwa hadhi kwa soko hilo kuwa mji, wakisema hatua hiyo itachochea ukuaji wa biashara zao na kuboresha mazingira ya kufanyia kazi. Hata hivyo, wametoa wito kwa serikali kuharakisha ujenzi wa soko la kisasa katika eneo hilo ili kuwaondolea dhiki wanazokumbana nazo kila mwaka wakati wa msimu wa mvua na jua kali.