Itamlazimu kila mkenya kumuwajibikia mwenzake, ikiwa taifa litaweza kushinda vita dhidi ya dhuluma za kijinsia kwa Watoto.
Ndiyo kauli ya katibu wa jinsia Ann Wang’ombe, aliyezuru nyumbani kwao Shantel waruguru, mtoto wa miaka 9 aliyenajisiwa, kuwaawa na mwili wake kutupwa chooni kijijini Rititi, eneo bunge la Mathira jumanne. Katibu huyo pia amezitaka asasi za usalama, kufuatilia kwa ukaribu ripoti zinazotolewa kwao na jamii za wale wanaokisiwa kuwa na mienendo iliyopotoka,ili kuzuia visa vya ubakaji wa Watoto,