- 765 viewsDuration: 2:29Maafisa wa DCI sasa wanadurusu faili za walimu wakuu na maafisa wa elimu wa kaunti wanaohusishwa na sakata ya shule bandia na kusajili wanafunzi hewa ili kupora fedha za umma. Waziri wa Elimu, Julius Migos Ogamba, amesema kuwa wahusika watafunguliwa mashtaka. Hayo yanajiri huku baraza la mtihani likitangaza tarehe za usajili wa wanafunzi watakaofanya mitihani ya kitaifa mwaka huu.