- 1,338 viewsDuration: 1:29Viongozi wa Upinzani wamekashifu kile wanachokitaja kuwa utoaji hongo kwa Wakenya katika ikulu ya Nairobi , wakisema unalenga kuwashawishi kumpigia kura rais william ruto kwenye uchaguzi wa mwaka wa 2027. Wakizungumza kwenye hafla tofauti nchini, Kiongozi wa PLP Martha Karua, mwenzake wa DAP-K Eugene Wamalwa na Aliyekuwa jaji mkuu David Maraga wanataka fedha zinazotolewa kwenye mikutano ya rais ikuluni zitumiwe kuboresha sekta ya elimu inayokumbwa na changamoto nyingi na ambapo sasa wahadhiri wa vyuo vikuu wamegoma.