Skip to main content
Skip to main content

Mtoto wa miaka miwili atoweka Kajiado katika kituo cha kutwa cha kulea watoto, familia yaomba msaada

  • | Citizen TV
    1,423 views
    Duration: 2:58
    Familia moja eneo la Kisaju kaunti ya Kajiado inahangaika baada ya mtoto wao wa miaka miwili kupotea kutoka kituo cha kutwa cha kulea watoto. Mamake mtoto aliyetoweka anasema kuwa msimamisi wa kituo hicho aliondoka kumpelekea mwanawe chakula shuleni na kuwaacha watoto watano kituoni, lakini mtoto huyo hakuwepo aliporejea. Familia ya mtoto huyo imekuwa ikimtafuta kwa siku 25 sasa bila mafanikio yoyote.