Maslahi ya walimu na utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu vilishamiri wakati wa sherehe za kitaifa za siku ya walimu duniani. Zaidi ya walimu elfu-3 walikusanyika mjini Nairobi leo kwa hafla hiyo, huku wakitoa wito wa kuajiriwa kwa walimu zaidi kwa masharti ya kudumu. Aidha, walihimiza serikali kushughulikia uhaba wa walimu, kupandishwa vyeo na utekelezaji bora wa mtaala huo mpya. Serikali imesema itaajiri walimu elfu-24 zaidi kufikia Januari 2026.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN
Follow us on Twitter: https://twitter.com/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1tv
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#KBCchannel1 #Kenya #News