Kufuatia kuwasilishwa kwa bajeti ya mwaka wa fedha wa 2026/2027 na waziri wa fedha John Mbadi, macho sasa yanaelekezwa mapendekezo kadhaa ambayo yanaweza kuwa na athari kubwa kwa walipa ushuru, biashara na sekta ya benki. Miongoni mwayo ni mabadiliko ya makataa ya kuwasilisha taarifa kuhusu ulipaji kodi. wafanyakazi wanaolipwa mishahara watahitajika kuwasilisha taarifa hizo kufikia mwezi Aprili kila mwaka. waziri Mbadi pia anapendekeza kuongezwa kwa muda wa mwisho kwa benki kukidhi hitaji la chini la mtaji wa shilingi bilioni 10 kuanzia mwaka 2029 hadi Desemba mwaka wa 2032.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive