- 69,265 viewsDuration: 3:58Jioni ya leo, kanda ya kipekee ya cctv imeonyesha matukio yaliyojiri kabla ya kifo tata cha kijana wa miaka 25 Festus Oromo katika jumba moja eneo la kilimani hapa Nairobi. Kwenye video, matukio yanaonyesha yaliyojiri kabla ya ugomvi kuzuka kati ya marehemu Festus na mwanamke aliyekuwa naye kwenye chumba cha kukodi saa saba ya usiku kabla ya mwili wake kupatikana chini ya jumba hilo.