- 572 viewsDuration: 3:27Na sasa tuangazie mila na desturi za jamii ya Turkana kwenye ndoa inayowahusisha watu wawili wasiokuwa wa jamii moja. Mwanaume anayeona msichana wa jamii hiyo sharti atimize matambiko kadhaa kama vile kuchinjwa kwa fahali maalum na kutenganishwa na bi harusi kwa siku mbili kabla ya kutoa mahari ya mbuzi na kupokezwa mkewe rasmi. Cheboit Emmanuel alihudhuria sherehe ya kitamaduni ambapo mwanaume mmoja kutoka jamii ya Waluhya alikuwa akimwoa msichana wa kiturkana na kuandaa taarifa hii.