- 4,881 viewsDuration: 3:29Familia sita za wanafunzi wa Chuo cha Laikipia zinalilia haki baada ya watoto wao kupigwa risasi na polisi wakati wa maandamano siku ya Jumatatu. Kijana mmoja mwenye umri wa miaka 19 alifariki wakati wa maandamano hayo huku wengine watano wakisalia hospitalini na majeraha ya risasi. Wanafunzi walikuwa wakiandamana kulalamikia kile walichodai ni utepetevu wa usimamizi wa chuo hicho kwa kukosa kufika haraka kumsaidia mwenzao aliyeanguka kwenye maporomoko yaliyotokea subukia siku ya Ijumaa.