- 1,771 viewsDuration: 3:17Familia moja kutoka eneo la Simba Cement, kaunti ya Kajiado inatoa wito kwa serikali na wahisani hasa mashirika ya kushugulikia majanga kuwasaidia kuutafuta mwili wa mtoto wao, aliyesombwa na mafuriko tarehe 6 mwezi uliopita, katika Mto Meruweshi, na hadi leo mwili wake haujapatikana. Juhudi za majirani na wakazi wa eneo hilo kuwasadia kuuopoa mwili huo hazijafaulu, walifanikiwa tu kupata mkoba na vitabu vya mwanafunzi huyo wa gredi ya sita, Robert Masai na Maelezo zaidi.