Gavana wa Kajiado, Joseph Ole Lenku, amewahimiza wakazi wa kaunti hiyo kujiunga na bima ya afya ya SHA ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za matibabu na kupunguza gharama .
Akizungumza wakati wa ziara yake katika eneo la Kajiado Kaskazini alikokagua miradi mbalimbali ya serikali ya kaunti ikiwemo shule ya ufundi ya Olekasasi hospitality ya saitoti na Olekasasi , aliahidi kuwa serikali ya kaunti itaendelea kuimarisha miundomsingi ya maji ili kuhakikisha wakazi wote wanapata maji safi na ya kutosha.