- 2,513 viewsDuration: 2:54Gavana wa Nyamira Amos Nyaribo hatimaye amejitokeza na kuzungumzia suala linalozingira kuzikwa kwa maiti katika kaburi la pamoja eneo la makaburini huko Kericho. Kulingana na Gavana Nyaribo, Kaunti yake iliidhinisha kuzikwa kwa miili 13 pekee kutoka Nyamira na kwamba maafisa wa Nyamira hawajui miili ishirini zaidi ilikotoka. Aidha, Nyaribo anasema kaunti yake ilitoa shilingi elfu 32 zilizohitajika kuzika maiti hizo huko Kericho.