Wakazi katika Kaunti ya Bungoma sasa wamepata afueni baada ya serikali ya kaunti hiyo kwa ushirikiano na serikali kuu kununua mtambo wa kisasa wa kupiga picha za matibabu CT-Scan.
Hatua hii inalenga kuimarisha huduma za matibabu na kuboresha utambuzi wa magonjwa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na yale yanayohitaji uchunguzi wa kina wa ndani ya mwili. Mtambo huo, ambao ni wa kwanza kuwekwa katika hospitali ya umma ndani ya kaunti hiyo, unatarajiwa kupunguza gharama na muda ambao wagonjwa hulazimika kutumia wakisafiri hadi kaunti jirani au hospitali binafsi kupata huduma hiyo.