- 3,076 viewsDuration: 2:55Wakenya ambao hawajajisajili kama wapiga kura sasa wana nafasi ya kufanya hivyo kuanzia Jumatatu, Machi 30, kwa kipindi cha siku thelathini. Hii ni baada ya Tume ya Uchaguzi, IEBC, kutangaza kuwa itaanza rasmi mchakato wa kuwasajili wapiga kura kote nchini, ikilenga kuwasajili wapiga kura wapya milioni 2.5. Haya yakijiri huku baadhi ya viongozi wakidai kuwa kuna wanasiasa wanaojaribu kuteka nyara mpango wa Niko Kadi, unaotumiwa na vijana kuwashawishi wenzao kujisajili kama wapiga kura.