- 634 viewsDuration: 2:40Katika eneobunge la Ugunja, ambako wakaazi kesho watamchagua mrithi wa waziri Opiyo Wandayi, Naibu mwenyekiti wa IEBC Fahima Abdalla ametoa hakikisho kuwa uchaguzi wa hapo kesho utakuwa wa haki, na kuwataka wakenya wanaohusika kuwajibika. Akizungumza baada ya kukagua shughuli ya usambazaji wa vifaa ya uchaguzi kaunti ya Siaya, Kamishna Abdallah aidha alisema tume hiyo inashirikiana na taasisi za usalama kuhakikisha uchaguzi huo hauna vikwazo.