- 999 viewsDuration: 3:02Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imetangaza kusajili wapiga kura wapya milioni 2.6 huku ikiwarai Wakenya ambao hawajajisajili kufanya hivyo katika vituo vilivyoko kwenye maeneo bunge. Bonde la Ufa linaongoza katika idadi kubwa ya wapiga kura wapya, likifuatwa na Mlima Kenya. IEBC hata hivyo inasema kuwa kutokana na uhaba wa bajeti, shughuli hiyo haitendelea zaidi ya mwezi mmoja ulioratibiwa.