Jaji Mkuu Martha Koome ametetea uhuru wa mahakama

  • | K24 Video
    4 views

    Jaji mkuu Martha Koome ametetea uhuru wa mahakama, huku akiwarai walio na malalamishi dhidi ya maafisa wa mahakama kuwasilisha kesi hizo mbele ya tume ya huduma za mahakama badala ya kufanya uchochezi hadharani. Koome pia amewaambia majaji, mahakimu na maafisa wengine wa mahakama waendelee kutekeleza majukumu yao bila uoga wala upendeleo. Vilevile, ametoa wito kwa wananchi kuwa katika mstari wa mbele kuilinda katiba. Koome amesema hayo leo baada ya Anne Amadi kumkabidhi paul ndemo mamlaka ya msajili wa mahakama katika mahakama ya milimani.