Skip to main content
Skip to main content

Kaunti 14 kwenye hatari ya kukosa fedha baada ya magavana kususia mwaliko wa kamati ya seneti

  • | KBC Video
    486 views
    Duration: 3:59
    Kaunti 14 ziko kwenye hatari ya kukosa mgao wao wa kipindi hiki cha matumizi ya fedha baada ya magavana husika kususia maagizo ya kufika mbele ya kamati ya bunge la seneti na badala yake kuelekea kwa mkutano wa faragha huko Kilifi. Kamati ya Uwekezaji wa Umma ya Kaunti katika bunge la Seneti imeonya kwamba itawasilisha ombi la kuzuiwa kwa ufadhili zaidi kwa kaunti za Lamu, Laikipia, Tharaka Nithi, Muranga, Embu, Baringo, Nandi, Siaya, Tana River, Nyandarua, Mombasa, Makueni, Elgeyo Marakwet na Kajiado baada ya magavana wao kukaidi mialiko ya kufika mbele ya bunge hiyo ili kuangazia jinsi walivyotumia fedha wakati wa mwaka wa fedha wa 2024/2025. Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/ #kbcchannel1 #news #kbclive