- 470 viewsDuration: 2:57Tume ya kitaifa ya kutetea haki za binadamu ya KNCHR inasema imethibitisha malalamishi kutoka kwa waathiriwa 1,800 wa visa vya ukiukaji wa haki za binadamu wakati wa maandamano. KNCHR ikipendekeza fidia ya shilingi milioni 3 kwa waliofariki na milioni 4 kwa waathiriwa wa dhuluma za kijinsia. Mwenyekiti wa tume hiyo Clair Ogangah amesema kuwa orodha hiyo itawasilishwa kwa rais William Ruto kabla ya kuanzishwa kwa zoezi la kuwafidia waathiriwa.