Makamishna walioteuliwa wa IEBC wasailiwa

  • | KBC Video
    32 views

    Kamati ya bunge ya kitaifa kuhusu haki na mswala ya sheria imewasaili watu wote saba waliopendekezwa kuwa makamishna wa tume huru ya uchaguzi na mipaka - IEBC. Aliyependekezwa kuwa mwenyekiti wa tume hiyo, Erastus Edung Ethekon, ambaye alikuwa mwanasheria mkuu kwenye serikali ya kaunti ya Turkana, alitakiwa kufafanua jinsi atakavyotekeleza wajibu wake bila upendeleo , hasa ikifahamika kwamba ana uhusiano wa karibu na naibu mkuu wa wafanyakazi katika ikulu ya rais, Josphat Nanok. Ethekon alijitetea akisema ana uwezo wa kuongoza tume hiyo akisema uhusiano wake na gavana huyo wa zamani wa Turkana ni wa kikazi na kwamba hautaathiri utendakazi wake.

    Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/

    #kbcchannel1 #news #kbclive