- 1,579 viewsDuration: 2:58Maseneta wa kamati ya seneti ya ugatuzi na mahusiano ya serikali, wameibua maswali kuhusu mkataba wa makubaliano, kati ya kaunti ya nairobi na serikali ya kitaifa, kuhusu ushirikiano wa utendakazi. Wanachama hawa wakidai kuwa serikali kuu imeipokonya mamlaka kaunti ya nairobi. Hata hivyo, akizungumza alipofika mbele ya kamati hiyo, mkuu wa waziri musalia mudavadi alitetea mkataba huo akisema uliafikiwa kulingana na katiba ili kuisadia kaunti ya Nairobi kupata fedha zaidi za maendeleo.