- 5,436 viewsDuration: 35sTazama jinsi mfanyakazi wa dukani nchini Mexico alivyomuokoa mtoto mmoja aliyekuwa akikimbia kuelekea barabarani wakati magari yakipita kwa kasi. Watu wengine pia walikuwa wakimkimbiza mtoto huyo ili kumuokoa, lakini mmoja wao alianguka na kushindwa kumfikia lakini mfanyakazi huyo yeye alifanikiwa kumfikia mtoto, akamshika na kujirusha naye pembeni mwa barabara hivyo kumzuia asigongwe na gari. Baada ya hapo, akamrudisha mtoto huyo salama kwa watu waliokuwa pamoja naye #bbcswahili #mexico #usalamabarabarani Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw