- 1,521 viewsDuration: 3:08Mvua inayoendelea kunyesha imekuwa kero kwa wakazi wa mitaa ya Bamburi na Kadzandani huko Mombasa. Usafiri katika barabara ya Mwembeni umekuwa kero huku biashara zikiathirika pakubwa, wakazi wakipata ugumu wa kufika katika kituo cha polisi na makazi yao. Na kama anavyoarifu Francis Mtalaki, wahudumu wa bodaboda na wakazi wanahofia mlipuko wa magonjwa kwa sababu ya ukosefu wa bomba la kupitishia maji.