- 195 viewsMwanamke mmoja kutoka mtaa wa Kibera hapa Nairobi sasa anaitaka serikali kumsaidia kumpata mwanawe aliyesalia nchini Saudi Arabia. Penina Wanjiru alikuwa akifanya kazi nchini humo ambako alilazimika kurejeshwa nchini kwa ghafla na mwajiri wake baada ya mtafaruku. Mwanawe wa miaka mitatu akilazimika kusalia kwenye kituo cha kuwalinda watoto, ila sasa ana wasiwasi wa maisha ya mwanawe, baada ya mawasiliano pia kukatika