- 11,333 viewsDuration: 3:29Kaunti kadhaa nchini zinajiandaa kukabiliana na msimu wa El Niño, huku baadhi zikijitahidi kurekebisha uharibifu uliosababishwa na mvua za mwaka jana kabla hali hiyo haijashuhudiwa tena. Kaunti ya Nairobi inasema imetambua maeneo 272 yaliyo katika hatari ya mafuriko, huku kukiwa na hofu kuwa huenda takriban watu laki moja, wakaathirika zaidi. Hata hivyo wataalamu wanasema mabilioni ya fedha yanayotumika kuboresha mifumo ya kupitisha maji hayatakuwa na maana, iwapo sheria moja muhimu itaendelea kupuuzwa;sheria inayotaka majengo kuwa angalau mita thelathini kutoka ukingo wa mto