Ndoa 70 za vijana wasio na mahari zafungwa Tanzania

  • | BBC Swahili
    645 views
    Ndoa 70 za vijana wasiokuwa na uwezo wa kutoa mahari zimefungwa kwa pamoja jijini Dar es Salaaam katika moja ya matukio nadra na adhimu kwa dini ya kiislamu nchini Tanzania. Zaidi ya shiling milioni 70 za kitanzania zimetolewa kama mahari kwa ajili ya vijana hao kutoka mikoa 12 ya Tanzania bara na Visiwani kati ya vijana zaidi ya 1,000 walioomba kusaidiwa kuoa. Mwandishi wa BBC Yusuph Mazimu alishuhudia tukio hilo na kuandaa taarifa hii #bbcswahili #tanzania #ndoa