- 135,470 viewsDuration: 2:23Orodha ya mashahidi wanaotajwa na Tundu Lissu imewakumbusha wengi tukio la mwaka 2012, wakati Rais Mstaafu Benjamin Mkapa alipofika Mahakama ya Kisutu kama shahidi katika kesi iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu. Mahalu alikuwa akikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi, yakihusisha ununuzi wa jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Italia na madai ya taarifa za uongo kuhusu thamani ya jengo hilo. Profesa Mahalu alipomtaja Rais Mkapa kuwa mmoja wa mashahidi wake, wengi hawakutarajia kumuona mahakamani. Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw