UWAJIBIKAJI NI UKAKAMAVU
Rais William Ruto amewatahadharisha vijana dhidi ya kuyumbishwa na shinikizo hasi la wana rika, akionya kuwa uhuru bila uwajibikaji ni utepetevu wa hali ya juu. Akizungumza wakati wa makala ya 95 ya msafara na ukaguzi wa kila mwaka wa shirika la St John Ambulance Kenya katika ikulu ya Nairobi, kiongozi wa taifa alikariri haja ya wajibu wa kiraia na uwajibikaji. Matamshi yake yanajiri huku kukiwa na madai ya kuandaliwa kwa maandamano yaliyopangwa kufanyika tarehe 25, mwezi huu ya ukumbusho wa wale walioangamia wakati wa maandamano ya kupinga muswada wa fedha wa mwaka-2024. Mwanahabari wetu Joseph Wakhungu anatuarifu zaidi.
#DarubiniWikendi
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive